

Shirika la Tanzania Safety Alliance (TASA) limeanza rasmi mfululizo wa mafunzo ya kuimarisha uwezo wa kitaasisi (Organizational Capacity Development) kwa lengo la kuboresha mifumo ya utendaji na uendelevu wa shirika.
Mafunzo haya yanayowezeshwa na Save the Children kupitia programu ya Vijana Plus, ni sehemu ya mkakati endelevu wa kutoa miongozo ya kiufundi kwa washirika wa maendeleo. Katika siku ya kwanza ya mfululizo huu, timu ya TASA imejikita katika mada za Mpango Mkakati (Strategic Plan) na Mpango wa Mwaka (Annual Plan) ili kuoanisha dira ya shirika na utekelezaji wa afua za mradi.
Lengo kuu la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa TASA inakuwa na mifumo madhubuti ya upangaji wa shughuli, usimamizi wa rasilimali, na upimaji wa matokeo ya muda mrefu. Kwa kuimarisha Mpango Mkakati, shirika linajiweka katika nafasi nzuri ya kutoa huduma zenye tija na zenye mwelekeo wa matokeo (Results-Based Management) kwa walengwa.
